MSINGI MKUU WA HUDUMA NI UPENDO
1. Ili huduma
zetu ziweze kupanuka na kukua ni lazima upendo wa kimungu utawale na kudumu
katika maisha yetu, pasipo upendo hata kama
utakuwa na huduma kubwa kiasi gani, lazima utashuka tu na kupoa. 1 Kor 13:1-8
Mungu alitumia upendo kwa kutukomboa kwa njia ya
upendo, ilibidi atoe kitu cha gharama kubwa (Yesu mwanae)
i. Huo
ulikuwa upendo wa gharama, upendo lazima uambatane na gharama kubwa, upate
hasara kwa mambo Fulani. Yh 3:16
ii. HUduma
nyingi zimekufa kwa sababu ya kukosa mbolea inayoitwa upendo
iii. Malumbano,
masengenyo, wivu na mafarakano katika huduma kwa sababu ya kukosa upendo ambao
ni tunda la Mungu
2. Mungu
aliweka Roho ya upendo ndani ya Mwanawe (Yesu Kristo). Hivyo huduma ya Yesu Kristo imejaa upendo
siku zote.
Yesu aliwapenda hata maadui zake na kuwaombea.
Sidhani kama unaweza kumwombea mtu unayemchukia n aunayemsema vibaya na
kutukana kwa maneno mengi.
i. Yesu
aliwapenda na kuwahurumia watu walioonewa na shetani, ndio maana huduma yake,
ilikuwa na nguvu siku zote, kwa sababu alitangaza UPENDO.
ii. YESU
aliona katika ulimwengu war oho chuki ni uuaji, ndio maana alisema watendeeni
mema wanaowaudhi na kuwanenea mabaya siku zote
iii. Yohana
anasema katika nyaraka, anayemchukia mwenzake ni muuaji na asiseme anampenda
Mungu, atawezaje kusema anampenda Mungu wakati anamchukia mwanadamu anayemuona
kwa macho, je, Mungu asiyemuona atawezaje kumpenda? Yh 2:9-11.
3. Upendo
huunganisha karama na huduma kuwa na nguvu, usione Mungu kakunyima huduma, au
karama. Maana ungemuona mwenzako sii kitu kwa kuwa kiburi na chuki kwa wengine
4. Mungu
anataka kupanda huduma ya upendo kwako, unasemaje kwa maana chuki imefanya
upokee matatizi, ugonjwa, huzuni, balaa, kugombana, vyeo vya duniani, kuuana kama Kaini alivyomuua ndugu yake. Hata watumishi wa Mungu
wengi wamekufa kiroho na kimwili, pia kwa sababu ya kukosa upendo wa kimungu
ndani yao,
wanagombania fedha madaraka nk
5. Kuanzia leo
ishi katika upendo kwa huduma uliyo nayo hata kama
unadharauliwa. Acha chuki utaona mkono wa Mungu ukikuinua na kukubariki. Amua
kukataa roho mbaya ya chuki, maana chuki ni uzao wa shetani. Na watumishi wake wa uzao wa Mungu, ni
upendo, amani, furaha, utu wema, fadhila,
na uaminifu.
Nakemea roho ya chuki kuanzia sasa, ichukie katika
jina la Yesu aliye hai Amina.
Ni mimi Rev Razaro emanuel Mpinga,
PO Box
103, Mbulu, Manyara,
Tanzania,
Afrika Mashariki.
No comments:
Post a Comment